Sunday, December 24, 2017

HASAD KATIKA NDOA 1

HASAD KATIKA NDOA:
 Baadhi ya watu hufanya chuki ama husda katika ndoa za watu kwa kutumia vitu mbalimbali, ikiwa kwa kusambaza maneno ya kuharibu kwa watu wa nje, ama familia ya mume au mke, wengine hufikia kutumia mpaka njia za kishirikina kwa lengo la kutaka kutafarakanisha (kuachananisha) ndoa za watu, sio wanadamu tu ambao hufanya uhasidi katika ndoa bali pia wapo hata majini ambao huleta mifarakano katika ndoa,husababisha ndoa za watu kuharibika.
BAADHI YA DALILI ZA NDOA ZILIZOHUSUDIKA:
   Zifuatazo ni dalili za ndoa ambazo zilizohusudika kwa namna mbalimbali ambazo husababishwa na maneno (fitna),ama kwa kutumiliwa njia za kishirikina zinazofanywa na binaadamu.
(1)"kuona mtu ambae huchukia  neema ambazo Allah (سبحنه وتعلى) amekuruzukuni katika ndoa yenu "
(2)"Kuona mtu ambae hufatilia na kutaka kuyajua yale ambayo yamo mpaka ndani ya ndoa yenu"
(3)"Ikiwa umekhitalifiana na mtu akawa ana kutishia amani katika ndoa yako"
(4)" Hata kuona mabadiliko kwa Mume/Mke ambayo ya sio mazuri na yaliyokuja kwa ghafla bila sababu kuijua"
(5)"Ikitokea umekhitalifiana (umekoseana) na mwanandoa mwenzako kwa khitilafi ndogo sana na ukaona ugomvi ni mkubwa bila ya kutarajia ugomvi huo kuwa itatokea kwa namna hiyo"
    Hizi ni baadhi ya dalili za ndoa ambazo zilizohusudika, ama  kwa baadhi ya dalili ambazo zinazosababishwa na  majini ni hizi zifuatazo.
BAADHI YA DALILI AMBAZO HUSABABISHWA NA MAJINI KATIKA KUTAFARAKANISHA NDOA:
(1)"Ikitokea kwa Mume kukosa nguvu wakati  watendo la ndoa na kujikuta usiku anapata ndoto za kufanya mapenzi na binti na akawa na nguvu".
(2)"Mke kukosa ladha ama utamu wa tendo kila unapofanya tendo la ndoa Mume"
(3)"Mume/Mke kutokuwa na hamu ya kuwa karibu na mwenzako kila mara"
(4)"Mume/Mke kuwa na hasira za ajabu ajabu kila unapokuwa na mwenzako"
(5)"Mme/Mke kuota kila mara ndoto za kufanya mapenzi".
    Hizi  ndio baadhi ya dalili ambazo husababishwa na majini ambao huleta husda katika ndoa, nini upi utatuzi wa matatizo haya.
UTATUZI:
     Ukiona matatizo haya yanakusibu kwa namna moja ama nyengine kinachotakiwa ni kumuelekea Mungu kwa kufanya dua za kumuomba yeye kuweza kukukinga na pia kukuondoshea haya matatizo, zipo dua mbalimbali za kufanya kumuomba Allah (سبحنه وتعلى) na akakuondoshea shida hizi ulonazo.
Ama wasiliana nasi ili tuweze kukusaidia kwa uwezo wa Allah(سبحنه وتعلى)
WASILIANA NASI
No:     +255676457532
Email:Alruqiyyatulshariyyah@gmail.com
           Yussufmohammed360gmail.com
Insta: sheikh_sharif_yussuft
You:   sheikh sharif yussuf
Blog:  sheikhsharifyusuph.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

SHEIKH SHARIF YUSSUF

HASAD KATIKA NDOA 1

HASAD KATIKA NDOA:  Baadhi ya watu hufanya chuki ama husda katika ndoa za watu kwa kutumia vitu mbalimbali, ikiwa kwa kusambaza maneno ya k...